Monday 31 July 2017

World Standards Day Celebrations - Tanzania Bureau of Standards

TAARIFA YA MKURUGENZI MKUU BW. JOSEPH B. MASIKITIKO KUHUSU MAADHIMISHO YA SIKU YA VIWANGO BARANI AFRIKA KATIKA NGAZI YA KITAIFA, ILIYOTOLEWA TAREHE 27 JANUARI, 2016
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) ni Shirika lenye dhamana ya kuandaa Viwango vya kitaifa na kudhibiti ubora wa bidhaa zinazozalishwa hapa nchini na zile zinazotoka nje ya nchi ili kumlinda mlaji na mtumiaji wa bidhaa hizo.
SGS Representative giving a word during press meeting Mr. Hemed
Katika kufanikisha hilo, TBS ni mwanachama wa  umoja wa waandaaji wa Viwango barani Afrika (ARSO), na maadhimisho ya siku ya Viwango katika ngazi ya bara la Afrika yanafanyika kila mwaka  kati ya mwezi Januari na Februari. Kauli mbiu  ya mwaka huu ni  Mchango wa Viwango Katika Kuwawezesha na Kuwaendeleza Wanawake yaani “How Standards Contribute to Women’s Empowerment and Development”



Tanzania kupitia TBS itakuwa mwenyeji wa mkutano mkuu wa Viwango barani Afrika mwaka huu ambao utaambatana na shughuli za maonyesho ya bidhaa za kitanzania yaani ‘made in Tanzania products’.
Vision Customer Service Manager Ms. Dorah updating visitors on event program
TBS kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini (TPSF) wameandaa maonyesho ya bidhaa za kitanzania ikiwa ni sambamba  na maadhimisho ya siku ya Viwango Afrika (ARSO) katika ngazi ya kitaifa, yanayotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 24  hadi 27 Februari 2016 katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.



 Maadhimisho hayo yanafanyika baada ya kuahirishwa kwa Sherehe za Siku ya Viwango Duniani zilizotakiwa kufanyika kitaifa kuanzia tarehe 9 hadi 13 Oktoba 2015 na kupangwa kusherehekewa wakati wa maadhimisho ya siku ya Viwango Afrika (ARSO) katika ngazi ya kitaifa.

Ushiriki wa mwaka huu utatoa fursa kwa makampuni mbalimbali kuonyesha bidhaa zao na kushiriki katika kupata bidhaa bora za Ki-Tanzania ikiwa ni maandalizi ya mashindano ya bidhaa katika ngazi ya bara la Afrika ili kupata “Made in Africa”.

Hii itafungua milango kwa bidhaa za Ki-tanzania kuingia katika masoko ya nje ya nchi pamoja na uhamasishaji kwa jamii ya Tanzania kununua bidhaa za Ki-Tanzania yaani bidhaa zinazozalishwa hapa nchini.

Pia lengo kuu  la maadhimimisho haya ni kuwakutanisha wazalishaji wa viwandani, wafanyabiashara, taasisi za Serikali pamoja na sekta binafsi   na kuzungumzia juu ya mchango wa Viwango katika kukuza biashara ndani na nje ya  nchi, kupanua mitaji, kuongeza ajira na kuboresha hali na maisha ya watanzania kwa kutumia bidhaa bora na salama.
 Maadhimisho haya yanatuandaa watanzania katika kuzitambua fursa za kibiashara zilizopo barani Afrika katika kuipeleka Tanzania kwenye ukanda huru wa kibiashara Afrika hapo mwakani yaani mwaka 2017.

Ikumbukwe kuwa mwaka  2017  umepangwa na umoja wa Afrika kama mwaka wa uimarishaji wa miundombinu ya ubora barani Afrika na hii imefikiwa na kikao cha wakuu wa  nchi za Afrika kilichofanyika Adis Ababa, Ethiopia  mwaka 2012 na kupanua biashara barani Afrika kwa asilimia  25 hadi 30.  Hii ni fursa muhimu kwa wazalishaji wa ndani kutumia nafasi hii adhimu katika kupanua masoko ya bidhaa zao.







Katika maonyesho hayo tunategemea mambo yafuatayo;
·      Wazalishaji wa ndani kuonyesha uwezo wao katika kutumia Viwango na kuzalisha bidhaa bora na salama,

·      Wajasiriamali kujifunza na kuzitambua fursa zilizopo katika utumiaji wa Viwango vya bidhaa katika kupata masoko, kuchochea uwekezaji pamoja na kupata mitaji,
 

·      Kushindanisha bidhaa kutoka kwa wazalishaji wakubwa, wa kati na wadogo  ili kupata bidhaa 50 au zaidi zitakazoshindanishwa wakati wa Mkutano mkuu wa ARSO mwezi Juni mwaka huu utakaofanyika jijini Arusha ambapo nchi zipatazo 35 zinatarajiwa kuhudhuria.

·      Bidhaa zitakazoshindanishwa wakati wa mkutano huo zitapata nafasi ya kushiriki kwenye mashindano ya ubora wa bidhaa yanayoandaliwa kila mwaka katika nchi za kusini  mwa  Afrika yaani SADC awards. Hii itafanya bidhaa za kitanzania kuingia kwa wingi kwenye soko la jumuiya ya SADC.

·      Bidhaa 20 zitakazochaguliwa mwezi  Juni zitashindanishwa kwenye mashindano ya bara la Afrika yanayotarajiwa kufanyika nchini Misri mwakani (2017).
  




Stall preparations

Maadhimisho haya yataleta chachu kubwa katika haya yafuatayo;

·      Kuchochea maendeleo  kwa kuongeza matumizi ya Viwango katika kutengeneza bidhaa na kutoa huduma mbalimbali nchini.
·      Kuongeza matumizi ya Viwango katika kutoa alama ya ubora.
·      Kuzitambua alama za ubora na faida zake kwa wafanyabiashara, wazalishaji na watumiaji wa bidhaa.
·      Kuhimiza matumizi ya bidhaa za ndani zenye  alama ya ubora.
·      Kujenga utangamano wa kibiashara  ndani na nje ya nchi.
·      Kuvutia wawekezaji na wafanya biashara kununua bidhaa za kitanzania zenye nembo ya ubora.
·      Kuongeza soko la nje.
Hivyo, tunawakaribisha kushiriki na kujifunza kuhusu Viwango pamoja na shughuli mbalimbali za kukuza biashara yako ndani na nje ya taifa letu katika maadhimisho hayo.


Aksanteni kwa kunisikiliza

No comments: